10:40 AM
0

HATIMAYE RAIS KIKWETE AMTANGAZA MRITHI WAKE RASMI

 
MWANANCHI
Hatimaye Rais Jakaya Kikwete amemtaja mrithi wake baada ya kuwataka wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM kumchagua mgombea urais anayekubalika ndani na nje ya chama hicho.

Kikwete alisema hayo jana wakati akifungua kikao cha Halmashauri Kuu kwenye ukumbi wa ofisi ya makao makuu ya chama hicho mjini hapa, unaojulikana kwa jina la White House.
Kauli hiyo imekuja wakati chama hicho kikiwa kwenye wakati mgumu kupata mgombea mpya baada ya Rais Kikwete kumaliza muda wake wa vipindi viwili vinavyokubalika kikatiba, huku kukiwa na ongezeko kubwa la nguvu ya upinzani.

Juzi, Kamati Kuu ya CCM iliwaachia huru makada wake sita waliotumikia adhabu ya miezi 17 ya kuzuiwa kujishughulisha na shughuli za uchaguzi baada ya kubainika kukiuka sheria za uchaguzi za chama hicho kutokana na kuanza kampeni mapema.

Miongoni mwa makada hao, wamo wanaopewa nafasi kubwa ya kupitishwa na chama hicho na ambao kambi zao zimekuwa zikipambana vikali na kuweka wasiwasi wa kuivuruga CCM.

Lakini Kikwete, ambaye ni mwenyekiti wa chama hicho, alionekana kufahamu hali inayoendelea na alitumia muda huo kueleza jinsi ambavyo CCM imejidhatiti kupata mgombea urais kwa kuzingatia maslahi ya chama hicho na ya Watanzania, akisema wakati wa kudhani mtu yeyote anayeteuliwa na chama hicho atachaguliwa na wananchi umeshapita.

Rais Kikwete alisema kikao cha Halmashauri Kuu kina umuhimu wake kwa sababu kitaamua ushiriki wa CCM katika Uchaguzi Mkuu na kutoa ratiba ya uteuzi wa wagombea wa chama hicho.
Rais Kikwete alisema watu wote wanachama na wasio wanacham wanasubiri kwa hamu uamuzi wa vikao vya juu vya CCM.

“Watanzania wote bila kujali itikadi zao wanaitazamia na kuitumainia CCM kutoa uongozi ulio bora kwa nchi yetu. Hali hii inathibitisha uleusemi wa Baba wa Taifa kwamba Rais anaweza kutoka chama chochotelakini rais bora atatoka CCM,”.
Alisema CCM inatakiwa kutambua na kuzingatia uzito wa wosia huo wBaba wa Taifa na kuhakikisha kuwa unatekelezwa kwa ukamilifu wake.

“Asiyesikia la mkuu huvunjika guu. Vikao vya Kamati Kuu, HalmashauriKuu ya Taifa na Mkutano Mkuu wa Taifa, vina jukumu maalumu la kuongozna kusimamia mchakato wa uteuzi ndani ya chama,  utakaotuwezeshkupata wagombea wanaofaa,”alisema.
“Wenye kukidhi kiu na matarajio ya wanachama wa CCM na wananchi waJamuhuri ya Muungano wa Tanzania ni sisi. Lazima tupate wagombewanaochagulika, tunapowapeleka kwa wananchi ambao wengi wao siywanaCCM.”
                                          
                                                                           www.mtumishijasiri.blogspot.com

0 comments:

Post a Comment

:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.