9:20 PM
0

Huu ndio mkanganyiko ulioko ndani ya baraza la senate uko Marekani juu ya sheria ya ugaidi

01 june 2015..mtumishijasiri

Baraza la Senate la Marekani limeshindwa kuzuia kumalizika kwa muda wa saa mbili wa sheria ya kupambana na ugaidi ambapo Shirika la Usalama wa Taifa linakusanya kwa wingi taarifa katika simu za raia wa Marekani.

 Katika mjadala wa Jumapili ambao ni nadra wajumbe wa Senate hawakukubali kuongezea muda wa kuendelea kwa sheria ya sasa ikiwepo migawanyiko miongoni mwa wajumbe wa chama cha Republican kwa kushindwa kuafikiana.

Baraza la Senate kwa sasa linajadili Muswada wa kuanzisha ufuatiliaji wa hatua za karibu zaidi.
Muswada ambao umekwisha pitishwa na Baraza la Wawakilishi.

Rais Obama na mkuu wa shirika la ujasusi la Marekani,CIA, John Brennan, wameonya kuwa kushindwa kupitisha upya kwa hatua za ufuatiliaji vitendo vya kigaidi kutaifanya nchi kushindwa kufuatilia vitisho vya kigaidi.
                                                mtumishijasiri.blogspot.com

0 comments:

Post a Comment

:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.